CORRECT LYRICS

Lyrics : Amepotea

Vipeperushi vinasambaaa
Eti natafutwa
Nimepotea, wiki imekata
Ndugu wamechachamaa
Wananitafuta
Nimepotea mwezi imekata

Kazini sionekani
Yupo wapi huyu
Simuni sipatikani

Yupo wapi huyu
Baba kaniuoizia
Yupo waapi huyu
Mama haishi kulia
Yupo wapi huyu

Mimi, nimezama katika kina
Kirefu cha bahari ya mapenzi
Nimezama katika kina
Kirefu cha bahari ya mapenzi
Sio mwana rahabu mlomkuta tanga

Sijafanywa msukule msipate tabu kumaliza waanga
Amenirudisha shule hesabu maumbo kupanga
Penzi lawa sasa mbule lenye protini vitamini na wanga
Aaah ladha yake, si sukari
Ni vichenza na malimao
Mechi zake huwa hatari
Ni chenga na mabao
Kazini sionekani
Yupo wapi huyu
Simuni sipatikani
Yupo wapi huyu
Baba kaniuoizia
Yupo waapi huyu
Mama haishi kulia
Yupo wapi huyu

Mimi, nimezama katika kina
Kirefu cha bahari ya mapenzi
(Msinitafute, msihangaike)
Nimezama katika kina
Kirefu cha bahari ya mapenzi
Nipo salama mimi, nipo salama mimi
Msinitafute niko salama mimi