CORRECT LYRICS

Lyrics : Kosa Langu

[VERSE 1]
Barua yako uliyotuma
kwa Ricardo Momo nimeisoma
Ila nimechelewa kuijibu
Sababu moyoni imenchoma
Nliyo yategemea
Tofauti na nlicho kiona
Hata naandika hii barua
Huku roho yangu inansonona
Umesema nichane nguo
Pia funguo umeirudisha sawa
Simu niziweke kituo
Na sio chaguo
Nikome kabisa sawa
Umesema hata ile picha nzuri
Nliyo kukumbatia
Niichane sawa
Ila kinachoniumiza
Mbona moja umesahau

[CHORUS]
Kosa langu kosa langu hujaniambia
Na kuniacha peke yangu ukanikimbia
Ila mbona kosa langu hujaniambia yeaaah
Nami nikabiki peke yangu ukanikimbia

[VERSE 2]
Mbona ukanichimbia kaburi ningari bado mzima
Niife nizikwe vizuri nipotee kabisa kimya
Licha ya matendo mazuri kwa upendo na heshima
Moto ukachochea tanuri ukachoma wangu mtimaa
Natamani hata ningepata nafasi
Muda wakati Kukutazama
Unione hata japo sura
Unitazame macho yangu mwenzako wimbi
limenipiga kasi
Langu jahazi limezama
Mnyonge mwana Sanura
Wee ndio ulikuwa furaha yangu

Tatizo hata nkilia
Wa kunifuta machozi sina
Sawa na gari lisio na gear
La kuiforce ipande mlima
Ndio maana siishi kulalama
Japo jibu moja tuu
Linaloniumiza mwenzio bado sijaelewa

[CHORUS]
Kosa Langu kosa langu (Kosa langu)
Hujaniambia (Hujaniambia)
Na kuniacha peke yangu (peke yangu)
Ukanikimbia (Ukanikimbia)
Ila mbona kosa langu (Kosa langu)
Hujaniambia  (Hujaniambia)
Nami nikabiki peke yangu (Peke Yangu)
Ukanikimbia (Ukaenda Ooh!)

Wasafi Records

(Oooh moyo)
Moyo wangu umevunjika una magongo
(Oooh moyo)
Kila sehemu nayoshika kinyamazongo
(Oooh moyo)
Hata chozi likifutika linabaki tongo
(Ooooh moyo)
Najitahidi kulidhika ila nna kinyongo

(Ooooh moyo) Moyo wangu umevunjika Unaa jamani
(Ooooh moyo) Hhhhmm hmm